Monday, July 21, 2014

SHULE YA WASIOONA IRENTE YAFANYA ZIARA YA MAFUNZO KATIKA HIFADHI YA ZIWA MANYARA


SHULE YA WASIOONA IRENTE YAFANYA ZIARA YA MAFUNZO KATIKA HIFADHI YA ZIWA MANYARA ILIYOFANYIKA TAREHE 9 – 11/7/2014


Shule ya msingi ya wasioona Irente yafanya ziara ya mafunzo katika Hifadhi ya Ziwa Manyara. Safari ilianza tarehe 9/7/2014 shuleni hapo na kuwasili Mto wa Mbu ambapo ndipo makao makuu ya Hifadhi hiyo yalipo.




Wanafunzi walipewa maelekezo mahali walipo na pana nini. Nilifurahi zaidi pale walimu walipoanza kuleza wanafunzi kwamba tunamalizia safu za milima ya Usambara na tunaanza safu za milima ya Pare. Mwalimu aliwambia wanafunzi kuwa kuna bonde lililotenganisha safu za milima ya Usambara na Pare. Mwalimu aliendelea kufafanua kuwa ukifuata bonde hilo utakutana na Hifadhi ya Mkomazi ambayo ipo katika mikoa miwili yaani Tanga na Kilimanjaro.


Mara baada ya kufika Hai mkoani Kilimanjaro wakaamua kupata chochote kwa uhai na ustawi wa mwili. Hivyo wakaingia katika Hoteli inayoitwa WESTLIFE VIP GARDEN

Tazama picha hapa chini.






Wanafunzi wakila chochote na kunywa katika Hoteli inayoitwa Westlife VIP Garden



Mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Ziwa Manyara walipokelewa vizuri na kuoneshwa mahali pa kulala. Wanafunzi waliwaona wanafunzi wengine waliofika Hifadhini hapo kwa Ziara za Mafunzo ambao nao waliitumia Hosteli hiyo hiyo. Walimu wakatoa elimu ya mazingira na ujongeaji kwani kwao yalikuwa mazingira mapya na yalihitaji uangalifu wa hali ya juu wakati wa kutembea.

Picha za hapa chini zinaonesha wanafunzi wakiwa katika Hosteli ya Hifadhi ya Ziwa Manyara






Hapa chini ni viwanja vya michezo vilivopo karibu sana na Hosteli ya Hifadhi ya Ziwa Manyara



                                         Wanafunzi wakifanya mazoezi kwenye bembea




Wananfunzi wakiwa na mwalimu wa Jiografia katika eneo la Chemchem ya Maji ya moto



Wanafunzi wakiwa eneo la Maji moto



Mwalimu wa Jiografia akishikilia fuvu la kichwa la nyani



Mwalimu mtaalamu akifurahia kuwepo kwenye eneo lenye maji ya chemchem ya moto



Nyani akiangalia wageni waliotembelea Hifadhi ya Ziwa Manyara

Wanafunzi wakipata chakula cha mchana ndani ya Hifadhi na kuwasikiliza waongozaji wakati wa kufanya majumuisho kwa makundi yote mawili

 Wanafunzi wakifurahia chakula cha mchana ndani ya Hifadhi






Wanafunzi na watalii kutoka nje ya nchi wakiwa katika eneo maarufu sana kwa wanyama aina ya VIBOKO

                                     Wanafunzi na watalii wengine wakigusa maji ya moto yatokayo ardhini



Twiga wakiwa katika maeneo yao ya kujidai

  Nyati na ndege wakiwa pamoja
Mkuu wa msafara akifurahia kuwepo muhimu ndani ya hifadhi

Aina mojawapo ya ndege wanaopamba Ziwa Manyara












Wanafunzi wakipapasa na kugusa ngamia Snake Park - Arusha

Geti ya kuingilia Hifadhi ya Ziwa Manyara


Wanafunzi wakigusa na kuchunguza kinyago cha tembo - Mto wa mbu

Mwalimu mkuu akiwagusisha wanafunzi baadhi ya silaha za jadi - Mto wa Mbu

Wanafunzi wakipapasa kinyago cha twiga akinyonyesha mtoto

Wanafunzi wakipapasa kinyago cha tembo - Mto wa Mbu

Wanafunzi wakifurahia kuona na kusikia mlio wa mamba - Snake Park Arusha

Nyani akisalimiana na wanafunzi  Snake Park Arusha

Mamba akiwa ndani ya wigo Snake Park Arusha







PONGEZI NA SHUKRANI
Tunapenda kutoa pongezi na shukrani kwa wadau wote waliofanikisha Ziara hii ya mafunzo katika Hifadhi ya Ziwa Manyara.

Mungu awabariki kwa moyo huu.

Kwa pamoja tutafanya makubwa zaidi

 

Damian Mkongwa

Mratibu wa Ziara

0784161644/753838499



















No comments :

Post a Comment