Wanafunzi wakimpapasa ngamia Snake Park Arusha
RIPOTI YA WANAFUNZI KUHUSU ZIARA YA MAFUNZO KATIKA HIFADHI
YA ZIWA MANYARA TAREHE 9 – 11/7/2014 SHULE YA WASIOONA IRENTE
Kwanza tunamshukuru Mungu
kwa kutuwezesha katika safari ile ya kutembelea HIfadhi ya Ziwa Manyara
tuliyoianza tarehe 9/7/2014 hadi 11/7/2014. Tunachoshukuru sana ni kwenda na
kurudi salama bila mtu au watu kuugua kwa maradhi au ajali.
Safari yetu ilianza saa
11:30 alfajiri na kufika saa kumi na moja jioni siku hiyo hiyo. Katika safari
hiyo tuliona na kusikia mengi ya kuvutia kama vile viwanja vya ndege kama KIA
na Kisongo – Arusha, Panone Super Market, kiwanda cha mkonge Mazinde, Hifadhi
ya Mkomazi, Chuo cha elimu maalum Patandi, Chuo kikuu cha Makumira, shule ya
viziwi Mwanga, Safu za milima Pare, Mlima Meru na mashamba ya maua Arusha.
Mapokezi: Tulipokelewa na wenyeji kwa ukarimu na wenyeji wetu
Manyara
Siku ya pili: Tuliingia
ndani ya Hifadhi ya Ziwa Manyara kuona wanyama waliomo pamoja na ndege. Wakati
tunaanza kutembelea hifadhi hiyo tulipewe historia fupi ya Hifadhi ya Ziwa
Manyara.
Historia ya Hifadhi ya Ziwa Manyara.
Hifadhi hiyo ilianzishwa
mwaka 1960 na Mheshimiwa Mbunge Barongo. Kabla ya mwaka 1960 ilikuwa ni eneo la
kuwindia wanyama na ndege. Mwaka 1958 uwindaji huo ulikomeshwa na kufanyika
kuwa hifadhi katika mwaka 1960. Neno Manyara limetokana na neno la Kimasai
liitwalo IMANYARA ambalo kwa Kiswahili ni mti uitwao MNYAA ambapo
kwa kisayansi unaitwa EUPHOBIA TURCALI na kwa jina la kawaida
linaitwa FINGER TREE.
Sifa ya Hifadhi ya Ziwa Manyara.
Kwanza hifadhi hiyo ina
ukubwa wa Km2 648.7. Hifadhi pekee yenye ndege wengi zaidi ya aina
30 wanaopamba hifadhi pamoja na Ziwa Manyara, Makundi ya wanyama zaidi ya saba
wanaoishi pamoja, Simba wanaopanda juu ya miti, Maji ya moto yanatoka kwenye
miamba na inapendwa kutembelewa na wanafunzi sana kwa miaka ya hivi karibuni.
Vivutio vilivyopo ndani
ya Hifadhi ya Ziwa Manyara.
Katika hifadhi hiyo kuna
vivutio vya aina nyingi na baadhi ya vivutio ni Maji moto ya chemchemi, miti
yenye sumu, maji ya ardhini yanayolisha misitu ndani ya hifadhi ambayo husaidia
kijani kuwepo karibu mwaka mzima, samba wanaopanda juu ya miti, Pundamilia,
Ngili, nyati, tembo, twiga, ndege, viboko, nyumbu, swala, mbuni fisi, duma,
pamoja na Ziwa Manyara nk.
Changamoto tulizopata
Changamoto tulizopata ni
pamoja na vumbi katika hifadhi ,usafi tulioukuta hauridhishi na tulipataa
pancha wakati wa kurudi.
Mafanikio
Pamoja na changamoto hizo
tumejifunza mambo mengi yakiwemo kujua kila tabia ya mnyama tuliemwona ,tulipata
historia ya hifadhi hiyo na kutambua chanzo cha ziwa Manyara. Pia tumeona na
kugusa vinyago vinavyochondwa Mto wa Mbu. Wakati tunarudi tulipitia Snake Park
Arusha ambapo eneo hilo lina nyoka, mamba, ndege, nyani, ngamia na vibanda vya makumbusho
SHUKRANI
Tunawashukuru
waliofanikisha safari hiyo,kwa pamoja tunasema Mungu awabariki.
Mwisho kabisa tunatoa
maoni yetu kwamba safari za mafunzo zisiwe mwisho bali ziwe endelevu kwani
wanafunzi wanajifunza kwa kugusa kunusa na kuona vitu halisi.
Ripoti hii imeandaliwa na
wanafunzi wa darasa la V – VII wa shule ya wasioona Irente
No comments :
Post a Comment